Wednesday, August 28, 2013

NGUZO ADILI ZA CHUO



WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI
CHUO CHA UALIMU KOROGWE
NGUZO ADILI ZA CHUO
1.Kibali cha kulala nje ya chuo, kumtembelea mwanachuo asiye wa jinsia yake bwenini, kutoka nje ya mipaka ya chuo, ua nyumbani kwa mfanyakazi hutolewa na mkuu wa chuo.
2.Kila mwanachuo sharti awahi darasani, mstarini, bwaloni/ukumbini, katika kazi za nje, mara aitwapo kwa kengele. Ni marufuku kwa mwanachuo kulala bwenini bila ya kibali cha mwadili na mganga wa chuo.
3.Ni marufuku kwa mwanachuo kumpotezea mwanachuo mwenzake muda katika mambo yasiyo na msingi hasa mikutano isiyo rasmi, vikao vya gizani, ulevi wa pombe, uasherati, bangi, madawa ya kulevya, kuishi kama mtu na mpenzi wake, kuasi na kukiuka taratibu za chuo.
4. Mwanachuo hatajishirikisha katika siasa wakati wote wa mafunzo yake hapa chuoni, anatakiwa kila wakati kutumia busara katika kufanya maamuzi yake, kutimiza wajibu kama utakavyoelekezwa na uongozi pamoja na wafanyakazi wengine wa chuo na uongozi wa serikali ya wanachuo, na kufuata kanuni na taratibu zote za serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
5.Mwanachuo hatakashifu, kuzomea, au kuguna wakati viongozi wa aina zote wa ndani na nje ya chuo wanapozungumza bali atauliza swali ili aelezwe zaidi, unapaswa kujiheshimu mwenyewe, kuwaheshimu wenzako, wakufunzi, wafanyakazi wengine pamoja na watu wengine utakaokutana nao. Jizuie kufanya jambo lolote litakaloleta tafsiri ya kuwadharau wengine.
6. Madai yote ya mwanachuo kutaka kubadili dini au jina akiwa chuoni hayatakubalika.
7. Mwanachuo atahudhuria masomo na vipindi vyote vya kujisomea na kufanya majaribio na mitihani yote ya chuo, kanda na taifa kwa bidii, utulivu, juhudi na maarifa.
8.Kwa usalama wa chuo ni marufuku kwa mwanachuo yoyote kupika bwenini au kukutwa na vifaa vyovyote vinavyoweza kuleta hatari ya moto bwenini kama vile jila la mafuta ya taa au umeme, heater, sufuria, pressure cookers n.k. Wanachuo wote wanapaswa kuondoka madarasani saa 4:30 usiku.
9.Mwanachuo atawapokea rasmi wageni wake kutoka ofisi ya zamu na kuwaelekeza taratibu za chuo zinazowahusu. Mwanachuo atabeba lawama zote endapo itabainika kuwa amesababisha matatizo au atakiuka taratibu za chuo. 
10.Kila mwanachuo anatazamiwa kujipenda, kuwa na maarifa na moyo wa kujituma, kutunza mali ya serikali, chuo na watu wengine. Kuvaa mavazi ya heshima na safi wakati wote, kutunza nywele vizuri, kutonyoa kipara, kufuga ndevu na sharafa, kuacha kucha ndefu na kuvaa mapambo yasiyoruhusiwa.
11.Mwanachuoharuhusiwi kuwa na mimba akiwa chuoni au kuja na mimba chuoni. Wanachuo wote yawapasa kuishi kama ndugu au kama kaka na dada hairuhusiwi kugombana au kupigana wakati wote wa mafunzo, ndani na nje ya chuo utapata kibali cha kutoka nje ya chuo na hataaibisha jina zuri la chuo kwa kuonekana kwenye majumba ya starehe na nyumba za kulala wageni

Mimi ……………………………………………………………………. Nakubaliana na nguzo adili zote za chuo. Naahidi kuzifuata kwa kipindi chote cha mafunzo yangu.

Sahihi ………………………………………………….                  Tarehe …………………………………………………………